Mamlaka ya Mapato Tanzania
Toggle Navigation
  • English
  • Maskani
  • Kuhusu TRA
    • Mkataba na mlipakodi
    • Dhamira na Dira ya TRA
    • Mpango Mkakati
    • Muundo wa Taasisi
    • Maadili kwa wafanyakazi wa TRA
    • Huduma ya barua pepe ya wafanyakazi wa TRA
  • Mawasiliano
  • Ajira
  • Zabuni
  • Minada
  • Mrejesho


         Bwana Alphayo J. Kidata

              Kamishna Mkuu

                           

Huduma za mtandao

  • Maskani
  • Jisajili kwa ajili ya TIN
  • Jisajili kwa ajili ya malipo
  • Tuma Taarifa ya VAT
  • Leseni za forodha
  • Usimamizi wa mizigo ya forodha
  • Usimamizi wa mashine za EFD
  • Jisajili kwa ajili ya kazi za Wasanii
  • Usaili wa Majengo

Viungo chapuchapu

  • Mashine za risiti za kielektroniki
  • Fomu
  • Pingamizi na rufaa za kodi
  • Ulipaji kodi
  • Raia wanaorejea nchini
  • Kuanzisha biashara
  • Kalenda ya matukio ya kodi
  • Riba, Adhabu ya ucheleweshwaji na Makosa

Maktaba

  • Sheria
  • Mikataba ya Kodi baina ya Nchi mbili
  • Maamuzi ya Kesi za Kodi
  • Machapisho
  • Takwimu za makusanyo ya kodi
  • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
  • Jedwali la Makato ya Kodi

Linki Linganifu

Chuo cha Kodi

Wizara ya Fedha na Mipango

Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji

Mamlaka ya Bandari Tanzania

BRELA

African Tax Administration Forum

Kenya Revenue Authority

Uganda Revenue Authority

Rwanda Revenue Authority

Office Burundais des Recettes

South African Revenue Service

  • Upo Hapa:  
  • Maskani
  • Mapato ya watu binafsi

 

UTOZWAJI KODI MAPATO WATU BINAFSI

Utozwaji wa kodi kwa watu binafsi umegawanyika katika makundi mawili. Kwanza, wafanyabiashara binafsi wadogo na ambao hawana uwezo wa kutunza kumbukumbu na kutengeneza hesabu za biashara zao. Pili wafanyabiashara wa kati wanaotakiwa na sheria kutunza kumbukumbu na kutengeneza na kuwasilisha hesabu zao kwa ajili ya kukadiriiwa. Wafanyabiashara wadogo wasio weza kuweka kumbukumbu hulipa kodi kwa mfumo wa makisio, na wafanyabiashara wa kati waliozidi kiwango cha mauzo cha Shilingi milioni ishirini kwa mwaka wanatakiwa kulipa kodi yao kwa kuzingatia faida ya mwaka iliyopatikana kutokana na ukaguzi wa hesabu zao za biashara zilizowasilishwa kwa Kamishna wa Kodi ya Mapato.

 

  • Mfumo wa Makisio ya Kodi

Huu ni mfumo wa kodi ambapo watu binafsi wasiokuwa na uwezo wa kutunza na kutengeneza hesabu za biashara hutozwa kodi kulingana na makisio ya mauzo yao kwa mwaka.  Mlipakodi aliye katika mfumo huu hatakiwi na sheria ya kodi ya Mapato kuandaa na kutuma hesabu za ukaguzi TRA. Hata hivyo, mlipakodi katika eneo atakapokuwa na uwezo wa kuweka vizuri kumbukumbu za biashara yake ana hiari ya kutotumia  mfumo  huu na  kuamua kuandaa hesabu za biashara yake zitakazotumika katika ukaguzi na  kukokotoa kiwango cha kulipia  kodi kulingana na faida aliyopata.

Masharti yanayokubalika ili ukadiriwe katika mfumo wa Makisio ya Kodi

 

  • Mlipakodi ni lazima awe mkazi
  • Mauzo ya mwaka yasizidi kiwango cha Sh. Milioni 100.
  • Mlipakodi awe amefanya biashara tu katika mwaka wa mapato na asiye na mapato mengine kama yatokanayo na ajira au uwekezaji. Kwa mfumo huu wa makadirio ya kodi, mapato ya mtu binafsi yanatakiwa yatokane na chanzo cha biashara pekee.  Endapo mapato yatapatikana kutokana na vyanzo vingine kama vile ajira na/au uwekezaji mlipa kodi atatakiwa kutengeneza mahesabu yatakayoyumika katika ukadiriaji wa mapato yake yote kwa jumla na hatoweza kukadiriwa kwa kutumia mfumo huu.

 

Viwango vya Kodi chini ya Mfumo wa makisio ya Kodi

Chini ya mfumo huu kodi inayolipwa itatokana na mauzo ya mwaka ya mlipakodi kama yalivyo tathiminiwa na Kamishna wa Kodi ya Mapato. Mauzo na viwango vya kodi vimeelezwa hapa chini:

Viwango vya kodi chini ya mfumo wa Makisio ya kodi

Viwango vya kodi kwa wafanyabiashara wadogo wakazi

Mauzo kwa mwaka

Uzingatiaji wa kifungu cha 35 cha Sheria ya Usimamizi wa Kodi (Utunzaji wa Kumbukumbu)

Asiyetunza Kumbukumbu  za kuridhisha

Anayetunza Kumbukumbu

za kuridhisha

Mauzo yasiyozidi

Sh. 4,000,000/=

Hakuna

Hakuna

Mauzo yanayozidi sh. 4,000,000/= na hayazidi Sh. 7,000,000/=

Sh.100,000/=

3% ya mauzo yanayozidi

sh. 4,000,000/=

Mauzo yanayozidi sh.7,000,000/= na hayazidi sh. 11,000,000/=

Sh.250,000/=

Sh. 90,000 + 3% ya mauzo yanayozidi sh.7,000,000/=

Mauzo yanayozidi sh.11,000,000/= na hayazidi sh. 14,000,000/=

Sh.450,000/=

sh. 230,000 + 3% ya mauzo yanayozidi sh. 11,000,000/=

Mauzo yanayozidi sh. 14,000,000/= na hayazidi sh. 100,000,000/=

Haihusiki

Sh. 450,000/= + 3.5 % ya mauzo yanayozidi

sh. 14,000,000/=

 

  Wafanyabiashara wanaoandaa hesabu za mizania

Hawa ni walipakodi ambao mapato yao ya mwaka yanazidi Sh. 100,000,000 na wanatakiwa kuandaa hesabu pamoja na taarifa za fedha katika biashara zao.

 

Kiwango cha kodi kwa watu binafsi wanaoandaa Hesabu za Ukaguzi

Walipakodi katika kundi hili wanalipa kwa kuzingatia faida wanazopata. Viwango vinavyohusika katika kundi hili ni kama ifuatavyo:

 Tanzania Bara

Mapato ya mwaka yanayotozwa kodi

Kiwango cha kodi

Ikiwa jumla ya mapato haizidi Sh. 3,240,000/=

HAKUNA

Ikiwa jumla ya mapato inazidi Sh. 3,240,000/= lakini haizidi Sh. 6,240,000/=

9% ya kiwango kinachozidi Sh. 3,240,000/=

 

Ikiwa jumla ya mapato inaizidi Sh. 6,240,000/= lakini haizidi Sh. 9,120,000/=

Sh. 270,000/= jumlisha 20% ya kiwango kinachozidi Sh. 6,240,000/=

Ikiwa jumla ya mapato inazidi Sh. 9,120,000/= lakini haizidi Sh.12,000,000/=

Sh. 846,000/= jumlisha 25% ya kiwango kinachozidi Sh. 9,120,000/=

Ikiwa jumla ya mapato inazidi Sh. 12,000,000/=

 

Sh. 1,566,000/=  jumlisha 30% ya kiwango kinachozidi Sh. 12,000,000/=

 

Zanzibar

Mapato ya mwaka yanayotozwa kodi

Kiwango cha kodi

Ikiwa jumla ya mapato haizidi Sh. 2,160,000=

HAKUNA

Ikiwa jumla ya mapato inazidi Sh. 2,160,000/= lakini haizidi Sh. 4,320,000/=

9% ya kiwango kinachozidi Sh. 2,160,000/=

Ikiwa jumla ya mapato inazidi Sh. 4,320,000 lakini haizidi Sh. 6,480,000/=

Sh. 194,400  pamoja na 20% ya kiwango kinachozidi Sh. 4,320,000

Ikiwa jumla ya mapato inazidi Sh.6,480,000 lakini haizidi Sh. 8,640,000/=

Sh. 626,400= pamoja na 25% ya kiwango kinachozidi Sh. 6,480,000

Ikiwa jumla ya mapato inazidi Sh. 8,640,000/=

 

Sh. 1,166,400/= pamoja na 30% ya kiwango kinachozidi Sh. 8,640,000/=

 

Ujazaji wa taarifa ya Mapato na ulipaji wa kodi

Maelezo ya makadirio ya kodi inayolipwa

Mlipakodi atatakiwa kutoa  taarifa ya awali ya mapato ambayo mlipakodi anatarajia kupata katika mwaka wa fedha na anapaswa kujaza na kuwasilisha ritani ya makisio hayo kwa Kamishna ndani ya miezi mitatu kuanzia mwanzo wa mwaka wa mapato (ambayo kwa watu binafsi utakuwa ni mwaka wa kalenda unaoanzia Januari hadi Desemba)

Aidha, mlipakodi huyo anatakiwa kuwasilisha na kulipa kodi ya makisio ya mwaka iliyokadiriwa katika kila robo ya mwaka wake wa mapato. Anapaswa kulipa kodi kwa awamu zisizozidi nne ambapo kila moja italipwa kila baada ya miezi mitatu. Tarehe za malipo ni kama ifuatavyo:

  • Mnamo au kabla ya tarehe 31 Machi
  • Mnamo au kabla ya tarehe 30 Juni
  • Mnamo au kabla ya tarehe 30 Septemba
  • Mnamo au kabla ya tarehe 31 Desemba

 

Fomu: ITX200.01.E – Maelezo ya Tathmini ya Makadirio- Mtu binafsi

Uwasilishaji wa taarifa ya mapato

Mlipakodi anapaswa kuwasilisha taarifa ya mapato ya mwaka kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania ndani ya miezi sita tangu tarehe ya kufunga hesabu za mwaka wa mapato.

Fomu:  ITX201.01.E Taarifa ya mapato –  Mtu binafsi

 

List of articles in category Kodi ya Mapato kwa watu binafsi
Title
Ni wakati gani Mtu binafsi anapaswa kuwasilisha taarifa ya mapato?
Ni vitu gani muhimu vya kuzingatia wakati wa kujaza taarifa yako ya mapato?
Ni kumbukumbu zipi zinapaswa kutunzwa na mlipakodi?
Je fomu za taarifa ya mapato zinahusisha nini?
Kuwasilisha taarifa ya mapato

Vikokotoo Vya Kodi

  • Kikokotoo cha Magari
  • PAYE Tanzania Bara
  • PAYE Tanzania Zanzibar

Rudi Juu

© 2022 Mamlaka ya Mapato Tanzania