Kodi ya Ongezeko la Thamani ni nini?
Kodi ya Ongezeko la Thamani ni kodi ya mlaji inayotozwa katika bidhaa zinazostahili kutozwa kodi, ikiwa ni pamoja na huduma, mali zisizohamishika na shughuli yoyote ya kiuchumi wakati wowote thamani inapoongezeka katika kila hatua ya uzalishaji na katika hatua ya mwisho ya mauzo. Kodi ya Ongezeko la Thamani inatozwa kwa bidhaa zote zinazozalishwa ndani na huduma na kwenye maduhuli. Kodi ya Ongezeko la Thamani anatozwa mtu aliyesajiliwa kulipa Kodi ya Ongezeko la Thamani tu.
Mawanda ya Kodi ya Ongezeko la Thamani ni yapi?
Kodi ya Ongezeko la Thamani itatozwa katika usambazaji wowote wa bidhaa, huduma na bidhaa zisizohamishika za shughuli yoyote ya kiuchumi Tanzania Bara ambapo ni usambazaji unaotozwa kodi unaofanywa na mlipa kodi katika shughuli ya kiuchumi anayofanya. Uingizaji wa bidhaa zinazokatwa kodi kutoka sehemu yoyote nje ya Tanzania Bara zitatozwa Kodi ya Ongezeko la Thamani na Sheria za Kawaida za Forodha na taratibu zitatumika. Bidhaa zote zitakazotumika nje ya Tanzania Bara hazitatozwa Kodi ya Ongezeko la Thamani baada ya kupata uthibitisho. Kodi ya Ongezeko la Thamani itatozwa kwa bidhaa na huduma zinazotozwa kodi. Viwango sanifu vya Kodi ya Ongezeko la Thamani ni 18% na 0% kwa bidhaa zinazosafirishwa nje ya nchi.