Faida ya mtaji kutokana na kupata riba katika ardhi na majengo.
Upatikanaji wa riba katika ardhi na majengo
Mtu anayepata riba katika ardhi au jengo atachukuliwa kama anapata mali pindi atakapoacha kupata riba hiyo ikiwa ni pamoja na wakati mali hiyo inapouzwa, inapobadilishwa, inapobadilishwa umiliki, inapogawanywa, inapobatilishwa, inapokombolewa, inapoteketezwa, au inaposalimishwa na katika suala la riba ya mali hiyo uwepo wake unapokoma, mara kabla ya kuwepo ukomo wa mali hiyo.
Sheria ya Kodi ya Mapato inamtaka mtu anayepata faida kutokana na kupata riba katika ardhi au majengo yaliyo katika Jamhuri ya Muungano, kulipa kodi ya mapato kwa awamu moja.