Tarehe Zipi ni Muafaka Kulipa Ushuru na Kodi?
Kodi za Mapato
· Kodi za zuio zinalipwa ndani ya siku 7 baada ya mwisho wa mwezi wa kalenda ambayo kodi hiyo inahusika.
· Kodi zinazolipwa kwa awamu (kodi zinazokadiriwa kwa awamu) zinazilipwa katika kila robo mwaka; kwa mfano walipakodi ambao vipindi vyao vya kulipa vinaisha tarehe 30 Desemba; awamu za malipo zitafikia wakati wa kulipwa mwishoni mwa Machi, Juni, Septemba na Desemba.
· Kodi ya kujikadiria italipwa tarehe ya mwisho ya taarifa ya mapato (miezi sita baada ya mwaka wa mapato)
· Kodi ya Kujikadiria Dharura inalipwa katika tarehe iliyobainishwa katika taarifa ya makadirio.
· Kodi Iliyorekebishwa inalipwa ndani ya siku 30 tangu tarehe ya makadirio.
. Kodi itokanayo na pato la ajira (PAYE) inalipwa ndani ya siku saba (7) baada ya kuisha mwezi wa kodi husika
. Kodi ya maendeleo ya ujuzi (SDL) inalipwa ndani ya siku saba (7) baada ya kuisha mwezi wa kodi husika
. Kodi ya bidhaa inalipwa ndani ya siku ishirini na tano (25) baada ya kuisha mwezi wa kodi husika.
. Kodi ya kidigitali.inalipwa ndani ya siku 20 baada ya kuisha mwezi wa kodi husika
Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT)
VAT inadaiwa na inalipwa kabla au kabla ya siku ya 20 ya mwezi unaofuata mwezi wa biashara ambayo mapato yanahusiana. Mlipakodi anahitajika kuwasilisha marejesho ikiwa mtu huyo ana kiasi halisi cha kodi ya ongezeko la thamani inayolipwa kwa kipindi hicho.
Kuongeza Muda wa Kulipa Kodi
Mlipakodi anaweza kuomba kwa maandishi kwa kamishna mkuu kuongezewa muda wa kulipa kodi kwa mujibu wa sheria.Kamishna mkuu kufuatia kupokea maombi hayo yakionyesha sababu ya msingi anaweza kusogeza tarehe ya kulipwa kodi au sehemu ya kodi. .
Kamishna mkuu atamjulisha mwombaji kwa maandishi, maamuzi juu ya maombi yake.Na pale ambapo kibali kimetolewa kwa kumruhusu mlipakodi kulipa kodi kwa awamu na mlipakodi ameshindwa kulipa awamu yoyote,kiasi chote cha deni la kodi jumlisha riba italipwa mara moja.
Kodi ya Mapato kwa Wasafirishaji wa Bidhaa na Abiria
Ushuru unaolipwa na mkazi anayehusika na usafirishaji wa abiria au bidhaa kwa mwaka itaamuliwa kwa mujibu wa viwango vilivyowekwa hapa chini
| Daraja A : Magari ya Abiria | |
Idadi ya Abiria | Kiasi cha Kodi |
Chini ya 5 | 120,000 |
6 hadi 15 | 250,000 |
Daraja B : Magari ya huduma za Kiutalii | |
Idadi za watalii | Kiasi cha Kodi |
0 hadi 15 | 650,000 |
16 hadi 25 | 900,000 |
26 hadi 45 | 1,300,000 |
46 hadi 65 | 1,800,000 |
Zaidi 65 | 2,400,000 |
Daraja C : Magari ya Mizigo | |
Uwezo (Tani) | Kiasi cha Kodi |
| Hadi 500kg | 120,000 |
Juu ya 500kg lakini chini ya tani 1 | 250,000 |
1 hadi 5 | 500,000 |
6 hadi 10 | 750,000 |
11 hadi 15 | 1,100,000 |
16 hadi 20 | 1,300,000 |
21 hadi 25 | 1,650,000 |
26 hadi 30 | 1,900,000 |
Zaidi ya 30 | 2,200,000 |
Daraja D : Vyombo vya moto Binafsi vya kukodi | |
Aina za vyombo vya moto | Kiasi cha Kodi |
Taxi | 180,000 |
Ride Hailing | 350,000 |
Ride Sharing | 450,000 |
Special Hire | 750,000 |
Habari & Matukio
IDRAS ITAONGEZA WIGO WA KODI NA KUSIMAMIA USAWA – CG MWENDA
MKUTANO WA TATHMINI YA UTENDAJI WA NUSU MWAKA
TRA YAKUSANYA TRILIONI 4.13 MWEZI DESEMBA PEKEE
IDRAS KULETA MAPINDUZI YA KIUTENDAJI TRA