Emblem TRA Logo

EFD/VFD na Risiti 

EFD ni mashine ya kutoa risiti za kielektroniki iliyothibitishwa na Kamishna Mkuu kwa matumizi katika shughuli za kibiashara.

VFD ni mfumo wa kidijitali (programu mtandao) ulioidhinishwa na Kamishna Mkuu kwa ajili ya kunakili, kusafirisha na kuhifadhi rekodi za data za mauzo kwa njia ya kielektroniki. Zote EFD/VFD zipo kwa ajili ya kutimiza malengo sawa kama vile, kuboresha ubora wa rekodi za biashara, kupunguza udanganyifu wa kodi, usawa katika kutathmini wajibu wa kodi, kupunguza migogoro ya kodi, na kuwezesha ufuatiliaji wa wakati halisi wa shughuli za kibiashara.

Risiti za kifedha ni risiti au ankara inayotolewa kwa kutumia kifaa cha kifedha, mfumo wa serikali wa malipo ya kielektroniki au mfumo mwingine wowote wa kielektroniki ulioidhinishwa na Kamishna Mkuu.

 

Wajibu wa Kupata na Kutumia EFD/VFD

Mtu anayetoa bidhaa, kutoa huduma au kupokea malipo kuhusiana na bidhaa zilizotolewa au huduma zilizotolewa ambaye mapato yake ya kila mwaka yanakadiria kuwa Tzs.11 milioni na zaidi atapaswa kupata na kutoa risiti ya kielektroniki au ankara ya kifedha kwa kutumia kifaa cha kifedha cha kielektroniki ambacho kitakuwa kimenunuliwa kutoka kwa Mtoa huduma aliyeidhinishwa.

  1. Watumiaji watakuwa huru kununua mashine ya Kielektroniki kutoka kwa mtoa huduma yeyote aliyeidhinishwa.
  2. Mtumiaji hataruhusiwa kuhamisha umiliki kwa njia yoyote EFD/VFD kwa mtu mwingine kwa sababu yoyote.
  3. Mtumiaji atahakikisha kuwa EFD/VFD inapatikana wakati wowote katika ofisi yake ya biashara na inonekana kwa urahisi.
  4. Pale mtumiaji anapokosea kuingiza data isiyo sahihi katika EFD yake au pale EFD inashindwa kufanya kazi kwa sababu yoyote, mtumiaji atapaswa ndani ya kipindi cha masaa ishirini na nne, kuripoti tukio hilo kwa mtoa huduma aliyeidhinishwa na Kamishna Mkuu.

     

Msambazaji wa EFD/VFD ni nani?

Ni chombo kilichothibitishwa na Kamishna Mkuu kwa kuagiza, kusambaza na kuuza EFD/VFD, kufunga, kuunda mipangilio, kuunganisha, kuwafundisha watumiaji jinsi ya kutumia EFDs na kutoa msaada baada ya mauzo ikiwa ni pamoja na matengenezo na huduma.

 

Mahitaji ya Kuidhinishwa kama msambazaji wa EFD/VFD

Mtaji wa chini ni shilingi bilioni moja na milioni mia tano za Kitanzania kwa watoa huduma wa vifaa vya kifedha vya kielektroniki na shilingi milioni hamsini za Kitanzania kwa watoa huduma wa vifaa vya kielektroniki vya mtandao.

  1. Timu ya kiufundi yenye ujuzi wa hali ya juu ili kufunga na kuunda vifaa vya kifedha, kufundisha na kusaidia watumiaji
  2. Uzoefu si chini wa miaka mitano katika kutoa vifaa vya kifedha au vifaa vingine vya teknolojia ya mawasiliano ya habari; na
  3. Mahitaji mengine yoyote kama yanavyoweza kuamuliwa na Kamishna Mkuu.

 

Orodha ya Wasambazaji wa EFD/VFD Walioidhinishwa